SUBRA (kusubiri)
Mwaanadamu kama
kiumbe wa Allah hakuachakuwa ni mwenyekupita katika mitihani mikumbwa ya  huzuni na hata furaha, kiasi kwamba njia
pekee ya kufaulu katika mitihani hiyo ni kushikamana tu na kamba ya Subra.  Mwenyezi mungu (S.W) anasema;
كُلُّ
نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ وَنَبْلُوكُم بِالشَّرِّ وَالْخَيْرِ فِتْنَةً
وَإِلَيْنَا تُرْجَعُونَ 
(Kila nafsi
itaonja mauti; na tunakujaribuni kwa shari na kheri. Na kwetu sisi mtarejeshwa. (Al-Anbiyaa
(17: 35). 
Subra ambayo
itamnufaisha mwanadamu ni ile tu, iliyojengwa juu ya misingi ya kisheria. Yaani
inayoendana na mafundisho sahihi, nayo ni muongozo wa Allah (S.W) na maelekezo
ya bwana mtume (SAW). 
Misingi ya subra
Subra  ijengwe juu ya misingi ya: 
a)   
Imani                 
  
b)   
Ikhlaaswi      
c)    
Kushukuru 
Bwana Mtume
(S.A.W)  anasema:
عجبا
لأمر المؤمن إن أمره كله خير ، وليس ذاك لأحد إلا للمؤمن ؛ إنأصابته سرّاء شكر؛
فكان خير له····
Ajabu  ya 
jambo  la  Muumin 
kwamba  kila  jambo 
lake  ni  kheri. 
Na halipatikani  hili  isipokuwa 
kwa  Muumin.  Anapofikwa 
na  jambo  zuri hushukuru nayo ni kheri kwake na
anapofikwa na jambo lenye madhara husubiri nayo ni kheri kwake))
Tahadhari
Wapo baadhi ya
watu wanamtazamo potofu juu ya mitihani ambayo Allah (S.W) huwajaribu waja
wake.  Kwa mfano, wapo wanaoamini kwamba, kwa
kadri mja anapopatwa na mitihani hasa ya kuondokewa na ndugu zake wa karibu,
upungufu wa mali, watoto na mithili ya hayo, ni kutokana na kukasirikiwa na
Allah (S.W).
Yapasa ieleweke
kuwa jambo hilo halitokuwa sahihi, na ni sawa na hadithi za sungura na fisi
tu.   Mtume (S.A.W) amesema:
            “Kutoka kwa Anas kwamba
Mtume   amesema:  ((Allaah Anapompendelea  mja 
Wake  kheri,  Humharakishia 
adhabu  duniani.  Na Allaah 
Anapomtakia  mja  Wake 
shari  Humzuilia  dhambi 
zake  hata Amlipe  Siku 
ya  Qiyaamah)). 
Na  amesema 
Mtume   (S.A.W):
            (Hakika malipo makubwa kabisa
yapo pamoja na mtithani mkubwa, na hakika Allaah Anapopenda watu Huwapa
mtihani. Basi atakayeridhika atapata radhi (za Allaah)na atakayechukia atapata
ghadhabu)) At-Tirmidhiy (Hadiyth Hasan Swahiyh).
“Aidha,
imesimuliwa, kutoka kwa Sa’iyd bin Abi Waqaasw (R.A) amesema: Nilimuuliza
Mtume (S.A.W): “Ee Mjumbe  wa  Allaah! 
Watu  gani  wanaopata 
mitihani  migumu  zaidi? Akasema: ((Mitume, kisha
mfano wake, na mfano wake. Hupewa mtihani mtu 
kulingana  na  Dini 
[imani] yake.  Ikiwa  Dini 
yake  ni  imara, 
mtihani wake  huwa  mkubwa. 
Na  ikiwa  Dini 
yake  ni  dhaifu 
hupewa  mtihani kulingana  na 
Dini  yake.  Husibiwa 
sana  na  mtihani 
mmojawapo  hadi atatembea ardhini
bila ya kuwa na dhambi)) At-Tirmidhiy (Hadiyth  Hasan 
Swahiyh) .
Vilevile,
kutoka kwa ‘Aaishah (R.A) (amesema: “Mtume  akisema: 
((Hakuna  msiba  wowote 
unaomsibu  Muislamu  isipokuwa tu Allaah Humfutia madhambi hata
mwiba unaomchoma)) Al-Bukhaariy na Muslim
SUBIRA NI SIFA ZA WAJA WEMA WA ALLAH
a)     
Nabii Ismail, Idrisa na Dhal Kifli. 
وَإِسْمَاعِيلَ
وَإِدْرِيسَ وَذَا الْكِفْلِ كُلٌّ مِّنَ الصَّابِرِينَ 
 “Na [taja] Ismaa’iyl na Idriys na
Dhal-Kifl, wote ni miongoni mwawenye kusubiri)) Al-Anbiyaa (17: 85).
b) Nabii Ayyub 
إِنَّا
وَجَدْنَاهُ صَابِرًا نِعْمَ الْعَبْدُ إِنَّهُ أَوَّابٌ 
 “Tumemkuta ni mwenye subira sana, uzuri
ulioje wa mja, hakika yeye ni mwenye
kurudiarudia kutubia [Kwetu])) (Swaad (38: 44).
b)     
Ulu-l azmi Mina rrusul
            ((Basi subiri [ee Muhammad]
kama walivyosubiri Mitume wenye ustahmilivu mkubwa)) (Al-Ahqaaf (46:
35).
Vigawanyo
vya  Subira
Subira
imegawika katika sehemu kuu nne:
1.     
Subira katika utiifu. Yaani kusubiri katika ‘amali anazotenda mja kwa kutumia mwili au
ulimi wake (kumdhukuru Allaahi). Allah ana sema;
وَاسْتَعِينُواْ بِالصَّبْرِ وَالصَّلاةِ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ
إِلاَّ عَلَى الْخَاشِعِينَ 
 ((Na tafuteni
msaada kupitia subira na Swalah; na hakika hilo ni kubwa isipokuwa kwa
Khaashi’iyn [wanyenyekevu])) Al-Baqarah (2: 45). 
Aidha Mwenyezi
mungu anasema katika Suuratu Twaahaa:
وَأْمُرْ
أَهْلَكَ بِالصَّلاةِ وَاصْطَبِرْ عَلَيْهَا لا نَسْأَلُكَ رِزْقًا نَّحْنُ
نَرْزُقُكَ وَالْعَاقِبَةُ لِلتَّقْوَى 
((Na waamrishe watu wako kuswali, na uendelee mwenyewe kwa hayo)) Twaahaa (20:
132).
2.     
Subira katika maasi. Kusubiri katika kuacha kutenda jambo lisilokuwa lenye kuridhisha kwa
kutumia mwili au ulimi wako.
3.     
Subira katika Qadhwaa (Yaliyopangwa) na Qadar (Yaliyokadiriwa) ya
Allaah. Kusubiri
katika kuizuia nafsi isiungulike au isimahanike au isighadhibike kutokana na
mitihani inayomsibu mja. Allah (S.W) anasema;
 . وَنَبْلُوكُم بِالشَّرِّ وَالْخَيْرِ
فِتْنَةً 
((Na
Tunakufanyieni mitihani kwa [mambo ya] shari na ya kheri))
Al-Anbiyaa (17: 35)
Katika suuratul
Al – Fajri  (89: 15 – 16 )Allah (S.W)
anasema;
فَأَمَّا الإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ
وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَن وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلاهُ فَقَدَرَ
عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ  
Ama binaadamu
anapojaribiwa na Mola wake, Akamkirimu na Akamneemesha,
husema: Mola wangu Amenikirimu!  Na ama
Anapomjaribu Akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Amenitia unyonge!”
Na katika
Suuratul-Baqara, Allah (S.W) anasema;
وَلَنَبْلُوَنَّكُمْ بِشَيْءٍ مِّنَ الْخَوْفْ وَالْجُوعِ وَنَقْصٍ
مِّنَ الأَمْوَالِ وَالأنفُسِ وَالثَّمَرَاتِ وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ··· 
Na bila shaka
Tutakujaribuni kwa kitu katika khofu na njaa na upungufu wa mali na nafsi na mazao. Na wabashirie wenye kusubiri. Wale ambao unapowafika msiba husema: (Innaa liLlaahi wa Innaa Ilayhi Raaji’uwn) “Hakika sisi ni wa Allaah na hakika sisi Kwaketutarejea”. Hao juu yao zitakuwa Baraka kutoka
kwa Mola wao na Rehma, na hao ndio wenye kuongoka)) Al-Baqarah (2:
155-157).
5. Subira kutokana na maudhi ya watu
Ni kuzuia
nafsi, ulimi na viungo visilipize maovu anayotendewa mtu.   
وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُواْ بِمِثْلِ مَا
عُوقِبْتُم بِهِ وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ 
((Na
mkilipiza [kuadhibu adui au Waumini] basi lipizieni [kuadhibu] kulingana na
vile mlivyodhuriwa. Na mkisubiri basi bila shaka hivyo ni ubora kwa wenye
kusubiri. 
وَاصْبِرْ وَمَا صَبْرُكَ إِلاَّ بِاللَّهِ وَلاَ تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ
وَلاَ تَكُ فِي ضَيْقٍ مِّمَّا يَمْكُرُونَ 
Na subiri. Na
kusubiri kwako kusiwe ila kwa ajili ya Allaah. Wala usihuzunike kwa ajil yao,
wala usiwe katika dhiki kutokana na hila wanazozifanya.  (An-Nahl (16: 126-127).
Katika Suuratu
– Luqmaan, Luqmaan anamuusia mwanawe;
يَا
بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ
وَاصْبِرْ عَلَى مَا أَصَابَكَ إِنَّ ذَلِكَ مِنْ عَزْمِ الأُمُورِ 
((Ee
mwanangu! Simamisha Swalah, na amrisha mema, na kataza maovu, na subiri kwa
yanayokupata. Hakika hayo ni katika mambo ya kuazimiwa) Luqmaan (31:
17) 
Kwa nini
subra?
i.                   
Wenye kusubiri ni wapenzi ya Allaah
((…na
Allaah Anawapenda wanaosubiri. Al- Imran 146))
ii.                 
Wenye kusubiri siku zote wapo pamoja
na Allaah: 
            (….hakika Allaah Yu Pamoja na
wanaosubiri . Al-baqara 246))
iii.               
Allaah    amewatunukia  bishara njema;  Baraka 
[na  Maghfirah],  Rehma 
Yake,  
            Na
bila shaka tutakujaribuni kwa kitu katika khofu na njaa na upungufu wa mali na
nafsi na mazao. Na wabashirie wenye kusubiri. Wale ambao
unapowafika msiba husema: Innaa liLlaahi wa Innaa Ilayhi Raaji’uwn. (Hakika
sisi ni wa Allaah na hakika sisi Kwake tutarejea)”. Hao juu yao
zitakuwa Baraka kutoka kwa Mola wao na Rehma, na hao ndio wenye kuongoka)
(Al- Baqara 155-157)
iv.               
Allaah  Ameahidi 
kuwalipa  malipo  mazuri 
kabisa  kwa sababu ya kusubiri
kwao.  
مَا عِندَكُمْ يَنفَدُ وَمَا عِندَ اللَّهِ بَاقٍ وَلَنَجْزِيَنَّ
الَّذِينَ صَبَرُواْ أَجْرَهُم بِأَحْسَنِ مَا كَانُواْ يَعْمَلُونَ 
            (Mlivyo navyo vitakwisha na
vilivyoko kwa mwenyezi Mungu ndivyo vitakavyobakia. Na kwa yakini Sisi
Tutawalipa ambao wamesubiri ujira wao kwa mazuri waliyokuwa wakitenda))
An-Nahl (16: 96). 
v.                 
Allaah   Ameahidi 
Maghfirah  na  ujira 
mkubwa  kwa wenye kusubiri na
wakatenda mema. 
إِلاَّ الَّذِينَ صَبَرُواْ وَعَمِلُواْ الصَّالِحَاتِ أُوْلَئِكَ
لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ كَبِيرٌ 
(Isipokuwa
ambao wamevumilia wakatenda mema, hao watapata Maghfirah na ujira mkubwa)
Huwd (11: 11).
vi.               
Allaah ameifanya  subira 
kuwa  ni  kinga 
kubwa  kwa maadui na hila zao,
kama walivyoaahidiwa Maswahaba katika vita vya Uhud. 
إِن
تَمْسَسْكُمْ حَسَنَةٌ تَسُؤْهُمْ وَإِن تُصِبْكُمْ سَيِّئَةٌ يَفْرَحُواْ بِهَا
وَإِن تَصْبِرُواْ وَتَتَّقُواْ لاَ يَضُرُّكُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئًا إِنَّ اللَّهَ
بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطٌ
(Na
ikikupateni kheri huwaudhi. Na ikikupateni shari wanafurahi. Na nyinyi
mkisubiri na mkawa na taqwa haitakudhuruni chochote katika hila zao. Hakika
Allaah kwa wayatendayo ni Mwenye Kuzunguka yote wayatendayo.
(Aal-‘Imraan (3: 120). 
Na Allah
ni mjuzi zaidi
