Saturday, June 7, 2014

RAISI ZUMA ALAZWA HOSPITALI.





Ofisi ya rais wa Afrika kusini imetangaza, Rais Jacob Zuma amelazwa hospitalini kwa ajili ya vipimo vya afya. 

Taarifa iliyotolewa na ofisi hiyo imesema madaktari wameridhika na hali yake, lakini hawakuendelea kutoa taarifa zaidi juu ya nini alichokuwa akiugua Rais Zuma. 

Siku ya Ijumaa Zuma alishauriwa kupumzika baada ya harakati kubwa za  kampeni ya uchaguzi na mpango wa mpito kuelekea utuwala mpya. 

Wiki mbili zilizopita rais huyo wa Afrika Kusini aliye na umri wa miaka 72 aliapishwa kwa mara ya pili kuwa kiongozi wa nchi hiyo baada ya chama chake tawala cha ANC kushinda uchaguzi wa May 7 kwa takriban asilimia 62 ya Kura

No comments:

Post a Comment