Saturday, June 7, 2014

KESI DHIDI YA MMOJA WA KIONGOZI WA NGAZI YA JUU YA IKHWANI MUSLIMIIN; MUHAMMAD BADIE KUTAJWA JULAI 5, 10 WAHUKUMIWA ADHABU YA KIFO.





Mahakama moja nchini Misri imewahukumu kifo wafuasi 10 wa chama kilichopigwa marufuku cha Udugu wa Kiislamu cha rais aliyepinduliwa madarakani Mohammed Mursi. 

Aidha, mahakama hiyo imeakhirisha hadi tarehe 5 Julai kutoa hukumu ya kesi inayomkabili kiongozi mkuu wa Ikhwanul Muslimin Muhammad Badie na watu wengine 38 wakiwemo maafisa wa chama hicho  

Kiongozi huyo wa Ikhwanul Muslimin ambaye tayari ameshahukumiwa adhabu ya kifo katika moja ya kesi zilizofunguliwa dhidi yake anakabiliwa pia na kesi nyengine zipatazo 40 ambazo nazo pia kama atapatikana na hatia atahukumiwa adhabu ya kifo. 

Kufuatia hukmu ya kifo ya wafuasi hao 10, Jaji Hassan Fareed ameiwasilisha hukumu hiyo kwa Mufti Mkuu wa Taasisi ya Ngazi ya Juu ya Kiislamu nchini humo ili iidhinishwe kama inavyotakiwa kisheria.

Wakati huohuo polisi wamewatia nguvuni wafuasi 15 wa Muhammad Morsi, Rais wa nchi hiyo aliyeondolewa madarakani, sambamba na kukaribia kuapishwa Abdel Fattah el-Sisi kuwa rais mpya wa nchi hiyo. 

Kuapishwa kwa El-Sisi kutarejesha tena madaraka ya utawala nchini Misri mikononi mwa afisa wa juu wa jeshi baada ya kupita miaka mitatu tu tangu mapinduzi ya wananchi yalipomng’oa madarakani aliyekuwa raisi wan chi hiyo Hosni Mubarak.

No comments:

Post a Comment