Saturday, June 7, 2014

WATUNISIA WATAKA UISLAMU UCHUKUE NAFASI KATIKA UTUNGAJI SHERIA ZA NCHI YAO



Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa na taasisi moja ya utafiti nchini Ufaransa yameonyesha kuwa Watunisia wengi wanaunga mkono Uislamu kuwa na nafasi katika utungaji sheria za nchi yao.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo wa maoni, asilimia 51 ya wananchi wa Tunisia wanaitakidi kuwa Uislamu unapasa uwe moja ya vyanzo vya utungaji sheria na uendeshaji serikali.
Asilimia 28 ya waliotoa maoni yao wamesema wanahisi ni bora dini isiwe na nafasi katika suala la utungaji sheria.
Hii ni katika hali ambayo asilimia 16 ya raia wa nchi hiyo wanataka Uislamu uwe ndio marejeo pekee ya utungaji sheria na uendeshaji wa serikali hiyo.
Kuhusiana na aina ya utawala, uchunguzi huo wa maoni aidha umeonyesha kuwa asilimia 52 ya raia wa Tunisia wanafadhilisha serikali yenye mfumo wa kidemokrasia kuliko mifumo mingineyo, wakati asilimia 26 ya waliotoa maoni yao wanapendelea mifumo mingine ya utawala badala ya ule wa kidemokrasia.
Kutokana na Watunisia wengi kutaka Uislamu uwe moja ya vyanzo vya utungaji sheria na uendeshaji serikali, imedhihirika kuwa wananchi hao wanaamini kwamba hakuna mgongano kati ya Uislamu na demokrasia na bila uislamu demokrasia haiwezi kusimama.

No comments:

Post a Comment