Thursday, June 5, 2014

SHEIKH MUHAMMAD HUSSEIN, MUFTI WA BAYTUL MUQADDAS AMEUONYA UTAWALA WA KIZAYUNI DHIDI YA KUKIVUNJIA HESHIMA KIBLA CHA KWANZA CHA WAISLAMU (MASJID AL-AQSWA)



SHEIKH MUHAMMAD HUSSEIN, MUFTI WA BAYTUL MUQADDAS AMEUONYA UTAWALA WA KIZAYUNI DHIDI YA KUKIVUNJIA HESHIMA KIBLA CHA KWANZA CHA WAISLAMU (MASJID AL-AQSWA)

Sheikh Muhammad Hussein, Mufti wa Baytul Muqaddas ameuonya utawala wa Kizayuni kwa kuendelea kuushambulia na kuuvunjia heshima msikiti wa kihistoria wa al Aqsa ambao ni kibla cha kwanza cha Waislamu.
Mufti huyo wa Baytul Muqaddas ametoa tamko akiutaka ulimwengu wa Kiarabu na ulimwengu wa Kiislamu kusimama imara kupambana na jinai za kila leo za utawala wa Kizayuni wa Israel na kulinda haki za taifa la Palestina na maeneo matakatifu.
Amesema, viongozi wa Israel wanapuuza vitendo viovu vinavyofanywa na walowezi wa Kizayuni katika msikiti wa al Aqsa, huku wanajeshi wa utawala huo dhalimu wakiendelea kuwazuia Wapalestina wasiotimiza miaka 50 kuingia hata katika eneo tu la msikiti huo.
Ni hivi majuzi tu, wanajeshi wa utawala wa Kizayuni walipouzingira msikiti huo kwa madai ya kipuuzi na kupiga marufuku ya kuingia na kutoka eneo hilo, ili kuwazuia Wapalestina kuingia sehemu hiyo takatifu.
Baada ya wanajeshi wa Israel kuuzingira msikiti wa al Aqsa, walowezi wa Kizayuni wakisaidiwa na wanajeshi hao, waliuvamia msikiti huo na kulivunjia heshima eneo hilo takatifu.
Lengo la Wazayuni la kuuvamia mara kwa mara na kuchimba mashimo na mahandaki pambizoni mwa msikiti huo, ni kukiharibu kikamilifu kibla hicho cha kwanza cha Waislamu eneo ambalo pia lina historia kongwe.
Kwa mujibu wa takwimu za taasisi ya Palestina ya Wakfu na Turathi za al Aqsa, tangu mwanzoni mwa mwaka huu wa 2014 hadi hivi sasa, Wazayuni 6311 wenye misimamo mikali wameuvamia msikiti huo na kuuvunjia heshima.
Wazayuni hao ni pamoja na walowezi wa Kizayuni, majasusi wa Israel pamoja na wanajeshi wa utawala huo dhalimu.
Mara nyingi uvamizi wa msikiti wa al Aqsa unafanywa na vikosi maalumu vya Israel na lengo lake ni kuwatia hofu Wapalestina wanafika eneo hilo kusali.
Taasisi ya al Aqsa imetoa takwimu hizo kwa kushirikiana na taasisi nyingine inayojulikana kwa jina la Taasisi ya Uimarishaji wa Msikiti wa al Aqsa na Matukufu yake.
Taasisi hizo za Palestina zimeonya kuwa, Wazayuni wamepanga kuendelea na jinai zao kwenye kibla hicho cha kwanza cha Waislamu, hivyo hatua za haraka zinatakiwa ili kuzuia jinai hizo.
Kwa upande wake Sheikh Abdul Adhim, Mkuu wa Baraza la Wakfu wa Kiislamu ambaye ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa masuala ya uimarishaji wa Msikiti wa al Aqsa ameashiria uvamizi wa hivi karibuni wa walowezi wa Kizayuni katika msikiti huo na kuitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka za kuliokoa eneo hilo takatifu la kihistoria.
Jinai za Wazayuni dhidi ya Wapalestina na dhidi ya matukufu ya Kiislamu zinatendeka huku madola ya Magharibi yakiendelea kuunga mkono kwa kila namna utawala wa Kizayuni wa Israel.
Hata hivyo fikra za walio wengi duniani zinazidi kuamka, na kadiri Wazayuni wanavyofanya jinai na dhulma dhidi ya Wapalestina, ndivyo hasira za walimwengu zinavyozidi kuongezeka dhidi ya utawala huo pandikizi.

No comments:

Post a Comment