Thursday, July 31, 2014

AL MADINA SOCIA SERVICE TRUST YAPONGEZWA KUWALISHA MAYATIMA!




Wananchi na wadau mbalimbali nchini wameipongeza Taasisi ya “Al–Madinah” kwa kujumuika kwa pamoja na zaidi ya watoto 500 walio katika mazingira magumu na mayatima katika kusherehekea siku kuu ya Eid l fitri.

Watoto hao kutoka katika vituo mbalimbali jijini Dare s Salaam walipata fursa ya kula na kufurahi kwa pamoja wakati wa karamu ya chakula cha watoto mayatima iliyoandaliwa na taasisi ya Almadinah Social Service Trust na kudhaminiwa na kampuni ya ufuaji wa umeme ya (IPTL).

Mkurugenzi wa taasisi hiyo Sheikh Ally Mubaraka aliyeandaa tukio hilo amesema, taasisi hiyo imegundua kuwa mayatima wengi hukumbwa na changamoto nyingi ambazo ni pamoja na mahitaji ya msingi yakiwemo chakula, makazi na malazi.

Wadau na wananchi mbalimbali jijini Dare s Salaam wameipongeza taasisi hiyo kwa tukio hilo la kuweza kuwakumbuka mayatima, na watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwani nao wanapaswa kufurahi kama watoto wengine katika maisha yao.

Aidha, wameziomba taasisi mbalimbali nchini kuiga mfano huo ili kuwaondolea simanzi na majonzi watoto hao, ili waweze kuishi katika hali ya furaha na amani kama watoto wengine.


No comments:

Post a Comment