Thursday, July 31, 2014

SHEIKH WA MKOA WA SINGIDA, SALUM MAHAMI AWATAKA UKAWA WAREJEE BUNGENI



Sheikh wa Mkoa wa Singida, Salum Mahami amewaomba wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kurejea bungeni na kuwapatia watanzania katiba itakayoendeleza amani na utulivu uliopo kwa miaka 50 ijayo.


Sheikh Salum ametoa nasaha hizo wakati akihutubia mamia ya waumini wa dini ya kiislamu wakati akizungumza na waumini hao katika uwanja wa Namfua mkoani hapo.


Amesema, UKAWA wasiporejea bungeni na kuendelea na msimamo wao, watakuwa hawaja watendea haki watanzania.


Amesema, wananchi wanashauku ya kuona wajumbe wote wamerejea katika meza ya kuijadili rasimu ya pili ya katiba ili kuwapatia watanzania katiba bora itakayowanufaisha wananchi wote.


Amesema, haoni sababu ya wajumbe wa bunge hilo maalumu kuendelea kuendelea kuvutana kwa hoja ya muundo wa serikali kuwa tatu au mbili kwani wenye haki ya kuamua muundo gani unawafaa watanzania ni wananchi wenyewe.


No comments:

Post a Comment