Friday, October 17, 2014

MAAMBUKIZI YA VVU KUTOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO YAPUNGUA TABORA



Maambukizi ya virusi vya Ukimwi (VVU), kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto yamepungua kwa asilimia 90.

Hayo yamesemwa na Meneja wa shirika la EGPAF Mkoa wa Tabora, Dk. Alphaxard Lwitakubi, mara baada ya Rais Jakaya Kikwete kukagua banda la shirika hilo katika maonyesho ya wiki ya vijana.

Lwitakubi, amesema lengo la EGPAF ni kufikia asilimia 98 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2015.

Amesema hatua hiyo itafikiwa endapo wanaume wataambatana na wake zao kwenda kwenye vituo vya afya kama inavyotakiwa, kwani hadi sasa zimefikiwa asilimia 48 kwa mwaka 2014 kutoka asilimia 5 mwaka 2010.

Dk. Lwitakubi, amesema Shirika la EGPAF limekuwa likijihusisha na kazi za kuzuia na kutokomeza maambukizi ya virusi vya Ukimwi (VVU), kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mawasiliano na Utetezi wa EGPAF, Mercy Nyanda, amesema katika huduma zao kumekuwa na mafanikio, kwani kwa sasa wajawazito wengi wanajifungulia vituoni tofauti hapo mwanzo.

No comments:

Post a Comment