Friday, October 17, 2014

MRADI MKUBWA WA KUBORESHA UMEME DAR KUKAMILIKA AGUST MWAKANI!



Mradi mkubwa wa megawati 80 kwa ajili ya kuboresha umeme katikati ya Jiji la Dar es Salaam unatarajia kukamilika Agosti mwakani.

Hayo yamesemwa na Kamishna Msaidizi wa Umeme, Innocent Luoga kwenye kikao kilichokutanisha Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Balozi wa Finland nchini, Sinikka Antila na ujumbe wake pamoja na wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini na taasisi zake.

Amesema mradi huo wenye thamani ya Sh bilioni 56 utaunganisha vituo vya kusambaza umeme katikati ya Jiji la Dar es Salaam ili kuhakikisha kuwa umeme haukatiki kabisa.

Ametaja vituo hivyo kuwa ni pamoja na Ilala, Kariakoo, Kituo cha Reli, Sokoine na Makumbusho na kuongeza kuwa mradi huo upo katika hatua ya utekelezwaji ambapo vifaa vya mradi vimeshapatikana pamoja na wataalamu kutoka Shirika la Umeme (Tanesco) kupatiwa mafunzo ndani ya nchi na nchini Finland.

Hata hivyo amesisitiza kuwa tayari wameshaanza kuzifanyia kazi changamoto hizo ikiwa ni pamoja na kuwakutanisha wadau wote wa mradi hususan Tanesco na Wakala wa Taifa wa Barabara Nchini (Tanroads).

No comments:

Post a Comment