Tuesday, June 21, 2016

SUBRA (kusubiri)



SUBRA (kusubiri)
Mwaanadamu kama kiumbe wa Allah hakuachakuwa ni mwenyekupita katika mitihani mikumbwa ya  huzuni na hata furaha, kiasi kwamba njia pekee ya kufaulu katika mitihani hiyo ni kushikamana tu na kamba ya Subra.  Mwenyezi mungu (S.W) anasema;
كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ وَنَبْلُوكُم بِالشَّرِّ وَالْخَيْرِ فِتْنَةً وَإِلَيْنَا تُرْجَعُونَ
(Kila nafsi itaonja mauti; na tunakujaribuni kwa shari na kheri. Na kwetu sisi mtarejeshwa. (Al-Anbiyaa (17: 35).
Subra ambayo itamnufaisha mwanadamu ni ile tu, iliyojengwa juu ya misingi ya kisheria. Yaani inayoendana na mafundisho sahihi, nayo ni muongozo wa Allah (S.W) na maelekezo ya bwana mtume (SAW).
Misingi ya subra
Subra  ijengwe juu ya misingi ya:
a)    Imani                    
b)    Ikhlaaswi     
c)     Kushukuru
Bwana Mtume (S.A.W)  anasema:
عجبا لأمر المؤمن إن أمره كله خير ، وليس ذاك لأحد إلا للمؤمن ؛ إنأصابته سرّاء شكر؛ فكان خير له····
Ajabu  ya  jambo  la  Muumin  kwamba  kila  jambo  lake  ni  kheri.  Na halipatikani  hili  isipokuwa  kwa  Muumin.  Anapofikwa  na  jambo  zuri hushukuru nayo ni kheri kwake na anapofikwa na jambo lenye madhara husubiri nayo ni kheri kwake))

Tahadhari
Wapo baadhi ya watu wanamtazamo potofu juu ya mitihani ambayo Allah (S.W) huwajaribu waja wake.  Kwa mfano, wapo wanaoamini kwamba, kwa kadri mja anapopatwa na mitihani hasa ya kuondokewa na ndugu zake wa karibu, upungufu wa mali, watoto na mithili ya hayo, ni kutokana na kukasirikiwa na Allah (S.W).

Yapasa ieleweke kuwa jambo hilo halitokuwa sahihi, na ni sawa na hadithi za sungura na fisi tu.   Mtume (S.A.W) amesema:
            Kutoka kwa Anas kwamba Mtume   amesema:  ((Allaah Anapompendelea  mja  Wake  kheri,  Humharakishia  adhabu  duniani.  Na Allaah  Anapomtakia  mja  Wake  shari  Humzuilia  dhambi  zake  hata Amlipe  Siku  ya  Qiyaamah)).
Na  amesema  Mtume   (S.A.W):
            (Hakika malipo makubwa kabisa yapo pamoja na mtithani mkubwa, na hakika Allaah Anapopenda watu Huwapa mtihani. Basi atakayeridhika atapata radhi (za Allaah)na atakayechukia atapata ghadhabu)) At-Tirmidhiy (Hadiyth Hasan Swahiyh).
“Aidha, imesimuliwa, kutoka kwa Sa’iyd bin Abi Waqaasw (R.A) amesema: Nilimuuliza Mtume (S.A.W): “Ee Mjumbe  wa  Allaah!  Watu  gani  wanaopata  mitihani  migumu  zaidi? Akasema: ((Mitume, kisha mfano wake, na mfano wake. Hupewa mtihani mtu  kulingana  na  Dini  [imani] yake.  Ikiwa  Dini  yake  ni  imara,  mtihani wake  huwa  mkubwa.  Na  ikiwa  Dini  yake  ni  dhaifu  hupewa  mtihani kulingana  na  Dini  yake.  Husibiwa  sana  na  mtihani  mmojawapo  hadi atatembea ardhini bila ya kuwa na dhambi)) At-Tirmidhiy (Hadiyth  Hasan  Swahiyh) .
Vilevile, kutoka kwa ‘Aaishah (R.A) (amesema: “Mtume  akisema:  ((Hakuna  msiba  wowote  unaomsibu  Muislamu  isipokuwa tu Allaah Humfutia madhambi hata mwiba unaomchoma)) Al-Bukhaariy na Muslim

SUBIRA NI SIFA ZA WAJA WEMA WA ALLAH
a)      Nabii Ismail, Idrisa na Dhal Kifli.
وَإِسْمَاعِيلَ وَإِدْرِيسَ وَذَا الْكِفْلِ كُلٌّ مِّنَ الصَّابِرِينَ
 Na [taja] Ismaa’iyl na Idriys na Dhal-Kifl, wote ni miongoni mwawenye kusubiri)) Al-Anbiyaa (17: 85).
b) Nabii Ayyub
إِنَّا وَجَدْنَاهُ صَابِرًا نِعْمَ الْعَبْدُ إِنَّهُ أَوَّابٌ
 Tumemkuta ni mwenye subira sana, uzuri ulioje wa mja, hakika yeye ni mwenye kurudiarudia kutubia [Kwetu])) (Swaad (38: 44).
b)      Ulu-l azmi Mina rrusul
            ((Basi subiri [ee Muhammad] kama walivyosubiri Mitume wenye ustahmilivu mkubwa)) (Al-Ahqaaf (46: 35).

Vigawanyo vya  Subira
Subira imegawika katika sehemu kuu nne:

1.      Subira katika utiifu. Yaani kusubiri katika ‘amali anazotenda mja kwa kutumia mwili au ulimi wake (kumdhukuru Allaahi). Allah ana sema;
وَاسْتَعِينُواْ بِالصَّبْرِ وَالصَّلاةِ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ إِلاَّ عَلَى الْخَاشِعِينَ
 ((Na tafuteni msaada kupitia subira na Swalah; na hakika hilo ni kubwa isipokuwa kwa Khaashi’iyn [wanyenyekevu])) Al-Baqarah (2: 45).
Aidha Mwenyezi mungu anasema katika Suuratu Twaahaa:
وَأْمُرْ أَهْلَكَ بِالصَّلاةِ وَاصْطَبِرْ عَلَيْهَا لا نَسْأَلُكَ رِزْقًا نَّحْنُ نَرْزُقُكَ وَالْعَاقِبَةُ لِلتَّقْوَى
((Na waamrishe watu wako kuswali, na uendelee mwenyewe kwa hayo)) Twaahaa (20: 132).
2.      Subira katika maasi. Kusubiri katika kuacha kutenda jambo lisilokuwa lenye kuridhisha kwa kutumia mwili au ulimi wako.

3.      Subira katika Qadhwaa (Yaliyopangwa) na Qadar (Yaliyokadiriwa) ya Allaah. Kusubiri katika kuizuia nafsi isiungulike au isimahanike au isighadhibike kutokana na mitihani inayomsibu mja. Allah (S.W) anasema;
 . وَنَبْلُوكُم بِالشَّرِّ وَالْخَيْرِ فِتْنَةً
((Na Tunakufanyieni mitihani kwa [mambo ya] shari na ya kheri)) Al-Anbiyaa (17: 35)
Katika suuratul Al – Fajri  (89: 15 – 16 )Allah (S.W) anasema;
فَأَمَّا الإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَن وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ  
Ama binaadamu anapojaribiwa na Mola wake, Akamkirimu na Akamneemesha, husema: Mola wangu Amenikirimu!  Na ama Anapomjaribu Akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Amenitia unyonge!”
Na katika Suuratul-Baqara, Allah (S.W) anasema;
وَلَنَبْلُوَنَّكُمْ بِشَيْءٍ مِّنَ الْخَوْفْ وَالْجُوعِ وَنَقْصٍ مِّنَ الأَمْوَالِ وَالأنفُسِ وَالثَّمَرَاتِ وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ···

Na bila shaka Tutakujaribuni kwa kitu katika khofu na njaa na upungufu wa mali na nafsi na mazao. Na wabashirie wenye kusubiri. Wale ambao unapowafika msiba husema: (Innaa liLlaahi wa Innaa Ilayhi Raaji’uwn) “Hakika sisi ni wa Allaah na hakika sisi Kwaketutarejea”. Hao juu yao zitakuwa Baraka kutoka kwa Mola wao na Rehma, na hao ndio wenye kuongoka)) Al-Baqarah (2: 155-157).

5. Subira kutokana na maudhi ya watu
Ni kuzuia nafsi, ulimi na viungo visilipize maovu anayotendewa mtu.  
     
وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُواْ بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُم بِهِ وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ
((Na mkilipiza [kuadhibu adui au Waumini] basi lipizieni [kuadhibu] kulingana na vile mlivyodhuriwa. Na mkisubiri basi bila shaka hivyo ni ubora kwa wenye kusubiri.

وَاصْبِرْ وَمَا صَبْرُكَ إِلاَّ بِاللَّهِ وَلاَ تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَلاَ تَكُ فِي ضَيْقٍ مِّمَّا يَمْكُرُونَ
           
Na subiri. Na kusubiri kwako kusiwe ila kwa ajili ya Allaah. Wala usihuzunike kwa ajil yao, wala usiwe katika dhiki kutokana na hila wanazozifanya.  (An-Nahl (16: 126-127).
Katika Suuratu – Luqmaan, Luqmaan anamuusia mwanawe;
يَا بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ وَاصْبِرْ عَلَى مَا أَصَابَكَ إِنَّ ذَلِكَ مِنْ عَزْمِ الأُمُورِ
((Ee mwanangu! Simamisha Swalah, na amrisha mema, na kataza maovu, na subiri kwa yanayokupata. Hakika hayo ni katika mambo ya kuazimiwa) Luqmaan (31: 17)

Kwa nini subra?
i.                    Wenye kusubiri ni wapenzi ya Allaah
((…na Allaah Anawapenda wanaosubiri. Al- Imran 146))
ii.                  Wenye kusubiri siku zote wapo pamoja na Allaah:
           
            (….hakika Allaah Yu Pamoja na wanaosubiri . Al-baqara 246))

iii.                Allaah    amewatunukia  bishara njema;  Baraka  [na  Maghfirah],  Rehma  Yake, 
            Na bila shaka tutakujaribuni kwa kitu katika khofu na njaa na upungufu wa mali na nafsi na mazao. Na wabashirie wenye kusubiri. Wale ambao unapowafika msiba husema: Innaa liLlaahi wa Innaa Ilayhi Raaji’uwn. (Hakika sisi ni wa Allaah na hakika sisi Kwake tutarejea)”. Hao juu yao zitakuwa Baraka kutoka kwa Mola wao na Rehma, na hao ndio wenye kuongoka) (Al- Baqara 155-157)
iv.                Allaah  Ameahidi  kuwalipa  malipo  mazuri  kabisa  kwa sababu ya kusubiri kwao.  
مَا عِندَكُمْ يَنفَدُ وَمَا عِندَ اللَّهِ بَاقٍ وَلَنَجْزِيَنَّ الَّذِينَ صَبَرُواْ أَجْرَهُم بِأَحْسَنِ مَا كَانُواْ يَعْمَلُونَ
            (Mlivyo navyo vitakwisha na vilivyoko kwa mwenyezi Mungu ndivyo vitakavyobakia. Na kwa yakini Sisi Tutawalipa ambao wamesubiri ujira wao kwa mazuri waliyokuwa wakitenda)) An-Nahl (16: 96).

v.                  Allaah   Ameahidi  Maghfirah  na  ujira  mkubwa  kwa wenye kusubiri na wakatenda mema.
إِلاَّ الَّذِينَ صَبَرُواْ وَعَمِلُواْ الصَّالِحَاتِ أُوْلَئِكَ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ كَبِيرٌ
(Isipokuwa ambao wamevumilia wakatenda mema, hao watapata Maghfirah na ujira mkubwa) Huwd (11: 11).

vi.                Allaah ameifanya  subira  kuwa  ni  kinga  kubwa  kwa maadui na hila zao, kama walivyoaahidiwa Maswahaba katika vita vya Uhud.
إِن تَمْسَسْكُمْ حَسَنَةٌ تَسُؤْهُمْ وَإِن تُصِبْكُمْ سَيِّئَةٌ يَفْرَحُواْ بِهَا وَإِن تَصْبِرُواْ وَتَتَّقُواْ لاَ يَضُرُّكُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئًا إِنَّ اللَّهَ بِمَا يَعْمَلُونَ مُحِيطٌ
(Na ikikupateni kheri huwaudhi. Na ikikupateni shari wanafurahi. Na nyinyi mkisubiri na mkawa na taqwa haitakudhuruni chochote katika hila zao. Hakika Allaah kwa wayatendayo ni Mwenye Kuzunguka yote wayatendayo. (Aal-‘Imraan (3: 120).
Na Allah ni mjuzi zaidi

No comments:

Post a Comment