Friday, May 12, 2017

HII NI MOJA KATI YA NDOTO ZANGU



Ibun jazar Islamic schools
NA INSHAALLAH IPO SIKU ITATIMIA.


Moja ya ndoto zangu ni siku moja kuiona Ibun Jazar ni shule moja miongoni mwa shule zinazofanikiwa na kusifika kwa matumizi ya Lugha ya Kiingereza na Kiarabu kama lugha za mawasiliano miongoni mwa wanafunzi, walimu na kwa watumishi wengine pia.
Huenda wakawepo wenyemawazo ya kuwa suala hilo haliwezekani, na wakajaribu kujenga hoja nyingi tu kuthibitisha madai yao. Ima kutokana na jitihada ambazo zimejaribiwa kuchukuliwa hapo awali na hatimaye kuonekana kushindwa kufanikisha suala hilo.
Napenda ieleweke kwamba kukosea kupo na sisi huenda tulikosea mapema kwa kutokuzingatia uteuzi wa watumishi kulingana na mahitaji ya Jazar yenyewe.
Aidha tumeshindwa kuieleza falsafa na mwelekeo wa Jazar kwa watumishi wetu jambo ambalo limefanya suala la kuzungumza Kiswahili ni jambo la kawaida na kamwe haliwezi kubadilika. Lakini alhamdu lillah, Jazar inabarka ya watumishi wake wengi wenye uwezo wa kuzungumza kiingereza au kiarabu na kizuri zaidi kunakitengo cha Qur`an ambacho masomo yake hufundishwa kwa kiarabu.
Vile vile uwajibikaji umekua ni tatizo kubwa, sio kwa Jazar tu bali kwa taasisi nyingi za kiislamu, unaosababishwa na mazoea katika kazi, baadhi ya watumishi kutokubali mapungufu yao, huku wakiamini kuwa siku zote wao ndio wanaopatia na wengine ni watu wa kukosea tu, kutokuaminiana katika mgawanyo wa majukumu, majungu kazini, kudhaniana vibaya na kutokufanya kazi kwa umoja.

Jitihada zetu za kupambana katika kutibu ugonjwa huu zimekua zikifeli kutokana na kujaribu kitibu ugonjwa usiofanyiwa vipimo, huenda daktari akakupa vidonge vya malaria lakini kumbe ulipoenda kupima katika zahanati nyingine ukagundulika ni maradhi yasiyohitaji vidonge hivyo.

Mara zote tumekuwa wakali sana kuwalazimisha watoto kuzungumza kiingereza au kiarabu wanapokuepo madarasani, lakini watoto haohao husikika wakizungumza Kiswahili katika halaqaat za qur`an, wanapokuwepo katika dahalia zao, wanapotumwa na walimu wao, wakati wa mapumziko au michezo, na huzungumza na walimu zao au watumishi wengine wasiokuwa walimu.
Kwa hakika hajulikani mwalimu wa kiingereza ni yupi, wa kiarabu ni yupi, mwalimu wa Qur`ani ni yupi, matron na hata patron. Wote wanazungumza Kiswahili.  Kwa hali kama hii gonjwa kwetu limekomaa kuliko kwa hawa watoto, hebu basi tutumbueni la kwetu haraka huku tukikamua kamua kwa watoto.

Kwa hakika haya ni maandalizi mabovu ambayo yanapaswa kukemewa na kila mtumishi ikiwa tunania ya kutengeneza na tuna malengo tuliyoyakusudia.

Kunahoja zinaweza zikajengwa kuwa mbona kuna baadhi ya shule sizo za bweni lakini ukifika watoto wanazungumza kiingereza na sio Kiswahili? Ni swali zuri sana ila kwa msomi wa lugha anafahamu (How community play the great role on language learning), lakini hata hao waliofanikiwa kwa njia kama hiyo ni baada ya kutengeneza mazingira ya ndani ya shule kuanzia kwa mlinzi, matroni, patroni, sekretari na walimu.
Lakini kama haya ni baadhi ya mapungufu, jee ndio tuseme tumeshindwa? Jee hakuna njia mbadala za kufanikisha hili? Jibu zipo njia mbadala nyingi tu za kufanikisha hilo.

Kwanza, umoja na mshikamano. Kutokana na muundo wa kituo cha Ibun Jazar kilivyo na miundo mbinu yetu ni lazima viongozi (walimu wakuu) kushirikiana na walimu wa lugha, walimu wa taaluma, walimu wa nidhamu, wakuu wa idaya ya lugha, matron na patron bila kujali upremari au usekondari, katika kulitekeleza hili.

Pili, Ipo haja suala hili liwekwe kama moja kati ya kosa la uvunjifu wa nidhamu kwa mtumishi na mwanafunzi atakaebainika akitumia lugha isiyokua kiingereza au kiarabu kwa maksudi. Iwe darasani, nje ya darasa, bwenini, na hata kipindi cha michezo maadamu bado yupo ndani ya eneo la shule.

Tatu, kuanzishwe masomo ya ziada ya lugha kwa watumishi na baadhi ya wanafunzi walio na matatizo au mapungufu katika matumizi ya lugha hizo.  
Ninaimani nitakua nimeeleweka kwa kiasi kikubwa. Haya ni mawazo yangu ninaweza nikapatia na pia kukosea. Kwa pale nilipopatia nauomba uongozi kwa upande wa Msingi na Sekondari kuyachukua mawazo haya na kuyafanyia kazi haraka iwezekanavyo. Na kwa pale nilipokosea, naruhusu kukosolewa na nakaribisha maoni mengine kwa nia ya kujenga na kuiendeleza Jazari na kuusaidida uislamu.
Aidha, Jambo hili litasaidia kupunguza mazaungumzo yasiyonaumuhimu (porojo) kwa wanafunzi na watumishi na kujikita katika kufanya kazi.
Mwisho nawaomba tufanyekazi kwa pamoja, upendo na mshikamano ili kufanikisha malengo yetu tuliyoyakusudia tukiamini kuwa Allah ndiye mlipaji.

Mkuu wa Idara ya lugha Sekondari 
 Mujbaraka Ghulaam ______________

No comments:

Post a Comment