Thursday, July 31, 2014

POLISI ALIYEFUKUZWA KAZI KWA UTOVU WA NIDHAMU AINGIA BAA NA SILAHA




Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime, mkoani Mara linamshikilia aliyekuwa askari polisi wa kituo cha Moshi, aliyefufukuzwa kazi mwaka 2012 kwa utovu wa nidhamu kwa kuingia katika ukumbi wa baa akiwa na silaha.

Mtuhumiwa huyo anashikiliwa kwa tuhuma za kukutwa na bunduki aina ya riffle ikiwa na risasi tano, ambayo ni mali Kampuni ya Ulinzi ya Paroma Security, anayotuhumiwa kuitumia kufanya uhalifu katika maeneo ya mgodi wa Nyamongo.

Kamanda wa Polisi Tarime, Lazaro Mambosasa, amethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo.

Amesema mtuhumiwa, alikuwa askari wa jeshi hilo Moshi, mkoani Kilimanjaro, na amekutwa akiwa na silaha hiyo baada ya kutoroka lindo lake na kwenda nayo katika ukumbi huo. 

Kamanda Mambosasa amesema kuwa Julai 29, walipata taarifa kutoka kwa raia wema za kuonekana mtuhumiwa maeneo ya Mtaa wa Magamaga, Kata ya Sabasaba, mjini Tarime akiwa na silaha hiyo yenye namba  58368 TZCAR 65963 ikiwa na risasi tano.

No comments:

Post a Comment