Thursday, July 31, 2014

WAISLAMU JIANDAENI UCHAGUZI MKUU 2015




Waumini wa dini ya Kiislam nchini wametakiwa kujiandaa kwa ajili ya kujiandikisha upya katika Daftari la Kudumu la Wapigakura katika zoezi linalotarajiwa kuanza rasmi Desemba, mwaka huu.

Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam, Sheikh Rajabu Katimba, ametoa wito huo katika Baraza la Idd El-Fitri, lililofanyika katika viwanja vya Mwembeyanga, jijini Dar es Salaam.

Amesema ni wajibu wa kila muislamu kujiandikisha katika daftari hilo ili kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Sheikh Katimba amesema awali ilidaiwa kuwa vitambulisho vya taifa ndivyo vitakavyohusika katika upigaji kura, lakini taarifa hiyo hazikuwa za kweli na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) yenyewe imezikanusha.

Nae, Mwakilishi wa Umoja wa Shule za Kiislamu, Sheikh Hashim Saiboko, amesema bado ipo dhuluma, ambayo inaendelea kutekelezwa kwa wanafunzi wa dini ya Kiislamu, hasa katika masomo ya dini.

Amesema masomo ya dini kwa sasa hayahesabiwi kwa wanafunzi wa kidato cha sita, hali inayosababisha wengine kushindwa kufikia malengo waliyojiwekea kutokana na somo hilo kutoingizwa katika rekodi ya alama

No comments:

Post a Comment