Friday, October 17, 2014

JAMII ZA WAFUGAJI ZAKABILIWA NA TATIZO LA KUZAA WATOTO WENYE VICHA VIKUBWA



Jamii za wafugaji zinadaiwa kukabiliwa na kiwango kikubwa cha tatizo la kuzaa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi unaochangiwa na wajawazito kukosa vitamini itokanayo na mboga za majani kutokana na kitoweo chao kikubwa kuwa nyama.

Katika hatua nyingine imeshauriwa miezi miwili au mitatu kabla ya kubeba ujauzito, mwanamke awe amepata vitamini aina ya follic acid ama kupitia ulaji wa mboga na matunda au kwa kupata vidonge maalumu kwa ajili ya kukabili tatizo hilo.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Chama cha Wazazi wa Watoto wenye Matatizo ya Mgongo Wazi na Kichwa Kikubwa (ASBAHT), Abdulhakim Bayakub katika mkutano na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es Salaam.

Bayakub pamoja na tatizo hilo, amezungumzia Maadhimisho ya Siku ya kupunguza uzao wa watoto wenye ulemavu huo amesema yatafanyika Oktoba 25 katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) jijini Dar es Salaam.

Amesema watoto wengi wamekuwa wakicheleweshwa kufikishwa hospitalini kutokana na sababu mbalimbali miongoni mwake ikiwa ni imani za kishirikina wakiamini kwamba tatizo hilo limetokana na uchawi.

No comments:

Post a Comment