Friday, October 17, 2014

SHILLING BILIONI 18 KUTUMIKA CHANJO YA SURUA



Serikali inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 18 kwa ajili ya chanjo ya surua na ribela inayotarajiwa kutolewa Oktoba 18 mwaka huu nchini kote.

Hayo yamesemwa na Ofisa mafunzo na mawasiliano wa idara ya kinga na chanjo wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Ibrahim Maduhu wakati wa mkutano wa kamati ya huduma ya afya ya msingi wa jiji la Tanga.

Amesema kuwa uwekezaji huo ni mkubwa kufanywa na serikali kwa wananchi wake kwa lengo la kuwapatia afya bora.

Dk Maduhu amesema, kuwa ni jukumu la kamati za afya nchini nzima
kuhakikisha wanaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa chanjo hiyo.

Naye mganga mkuu wa jiji hilo, Dk Asha Mahita amesema, kuwa asilimia 15 ya watoto waliopatiwa chanjo ya surua katika jiji hilo hawajajenga kinga kamili.

No comments:

Post a Comment